Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 25, 2010

Kituko vya mwaka - Waumini wakesha wakisali ili Wachungaji wao wafufuke!!

Waumini wa kanisa moja la Pentekoste magharibi mwa Kenya wamegoma kuwazika wachungaji wawili wa kanisa hilo waliofariki kwa ajali ya gari wiki moja iliyopita na wamekuwa wakisali mbele ya majeneza yao muda wote wakiamini kuwa watafufuka kama alivyofufuka YESU.Mchungaji Patrick Wanjohi na mchungaji Francis Kamau Ndekei, walifariki februari 15 mwaka huu kutokana na ajali mbaya ya gari lakini waumini wao wamekuwa wakiamini kuwa wachungaji hao wamelala tu na wala hawajafariki."Hatutawazika kamwe, kwakuwa hawajakamilisha misheni zao hapa duniani, tunawahitaji warudi duniani kumalizia majukumu yao kwani bila ya wao kanisa litakufa", alisema mmoja wa waumini hao.Awali uongozi wa kanisa hilo ulisema kuwa wachungaji hao watafufuka siku ya jumamosi na kuwafanya maelfu ya watu washinde kwenye mvua kubwa sana wakisubiria wachungaji wao wafufuke. Hata hivyo siku ya jumamosi ilimalizika bila wachungaji hao kufufuka.Mamia ya waumini bado wanaendelea kusali masaa yote mbele ya majeneza ya wachungaji hao wakisubiria miujiza ijitokeze na wachungaji hao wafufuke.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote