Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, February 24, 2010

Mbaroni kwa Kumuhifadhi Mtuhumiwa

JESHI LA POLISI Dar es Salaam limewakamata watu watano kwa kosa la kumuhifadhi raia wa Uingereza Salim Maunga [35] aliyekamatwa Uwanja wa NDege akiwa na dawa za kulevya. Watu hao inadaiwa ni rafiki wa mtuhumiwa huyo na ilidaiwa walimuhifadhi nyumbani kwao Makumbusho jijini Dar es Salam na kumsaidia katika sakata kusafirisha dawa hizo.Salim alikamatwa wiki iliyopita katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kubeba kete 69 za dawa za kulevya aina ya Cocaine na bangi gramu 610.Alikamatwa akiwa katika hatua ya mwisho ya ukaguzi kabla ya kupanda ndege ya British Airways, pia rafiki wa mtuhumiwa huyo waliandaa dawa za kulevya bandia pamoja na Sh3 milioni kwa ajili ya kumpa mtunza stoo wa kituo cha polisi uwanja wa ndege.Mara baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo aliyekuwa na hati ya kusafiria yenye namba 109483453, Kamishna Msaidizi wa polisi wa viwanja vya ndege nchini, Mwajuma Kiponza alisema walimpekua na kubaini kuwa alificha kete 16 kwenye pindo la suruali yake sehemu ya kiunoni na kete 14 zilikutwa katika pindo ya chini ya suruali yake.Pia alipofikishwa kituoni kwa ajili ya kumhoji zaidi walipofungua begi lake walikuta pia vinyago vitatu ambavyo alivibeba kinyume na sheria. Hivyo watu hao wameshikiliwa na Jeshi hilo kwa kosa la kumuhifadhi raia huyo huku wakijua dhamira ya rafiki yao huyo kusafirisha madawa na kushirikiana nae katika kufanya uhalifu huo ili aweze kusafirisha madawa hayo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote