Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, February 24, 2010

Marekani yaiokoa Meli ya Tanzania

Meli I ya kivita ya Marekani imefanikiwa kuzuia shambulizi kwa meli ya Tanzania kutoka kwa maharamia wasiojulikana, na kuwadhibiti wanane waliokuwa katika mchakato huo,Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umesema. Meli hiyo ya kimarekani, USS Farragut ilirusha helkopta SH-60B Seahawk na kwenda kuiokoa MV Barakaale 1 baada ya kupokea ishara zikiashiria kuwa meli hiyo, iko kwenye hatari ya kushambuliwa na genge la maharamia, taarifa ya ubalozi huo imesema. "Helkopta hiyo ilifanikiwa kufyatua risasi za tahadhari juu ili kuidhibiti boti iliyokuwa ikiongeza kasi ya kuiendea meli ile" ilisema. "Timu ya wanajeshi toka USS Farragut walijotosa kwenye boti ile na kuwakamata maharamia wanane waliokuwepo na kuwasafirisha kwa the Farragut." Hata hivyo, taarifa hiyo iliyochapishwa na Shirika la Habari la Reuters haikusema lini na wapi tukio hilo limetokea na pia halikubainisha uraia wa maharamia hao. The USS Farragut ni maalum kwa ajili ya kufanya maangalizi na ni sehemu ya kikosi maalum namba 151 ambacho kinafanya doria katika rasi ya Aden na mashariki ya pwani ya Somalia. Kikosi hicho maalum, kilianzishwa mwaka 2009, kinahusisha jozi tatu za meli kutoka Australia, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Pakistan, Canada, Denmark, Uturuki, Marekani na Uingereza miongoni mwa nchi washirika. Pwani ya Somalia ni miongoni mwa eneo hatari sana duniani kwa meli kusafiri. Idadi ya mashambulizi ya maharamia duniani kote yamepanda kwa asilimia 40 mwaka jana, ambapo maharamia wenye silaha walioshindwa katika mataifa ya pembe ya Afrika yanafikia karibu nusu ya matukio 406 yaliyoripotiwa kwa mujibu wa the International Maritime Bureau.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote