Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, February 17, 2010

Sherehe za Valentine zampeleka Ahera

HAMIS Said (22), mkazi wa Ukonga Stakishari, amekufa baada ya kuzidiwa na maji wakati akiogolea katika bwawa la Pub iliyojulikana Kiota. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, amesema tukio hilo lilitokea majira ya saa 4 usiku, huko maeneo ya Ukonga Stakishari.Amesema kuwa kijana huyo alikuwa ni mteja katika baa hiyo na alikwenda kwa ajili kupata vinywaji katika baa hiyo na baadae kuhitaji huduma hiyo ya uogeleaji.Amesema ilidaiwa kijana huyo wakati akiogelea alizidiwa na maji hayo na baadae maiti yake kukuta ikiogelea majini humo.Maiti imehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya Amana na polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi wa tukio hilo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote