Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, February 23, 2010

Mauaji ya Musoma hadi sasa watu 17 Mbaroni

Hadi kufikia jana mchana, jeshi la polisi nchini limefanikiwa kukamata watu 10 mkoani Mara wanaohusishwa na mauaji ya watu 17 wa ukoo mmoja.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Robert Boaz, amesema hadi sasa watu hao wameshakamatwa na msako mkali unaendelea ili kuhakikisha watu wote waliohusika katika kufanya unyama huo wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.Kamanda Boaz alisema watu hao walikamatwa katika maeneo tofauti ndani na nje ya mkoa huo baada ya kupata taarifa za uhakika kutoka kwa raia wema ambazo zimekuwa zikifanyiwa kazi na jeshi lake.Pia amewataka wananchi kuzidi kutoa taarifa kwa siri kuhusiana na watu hao.Amesema timu kubwa ya askari wake wamesambazwa kila kona ya mkoa wa Mara na nje ya mkoa ili kuwasaka watu hao wauaji na kusema kazi hiyo itafanikiwa kwa jeshi hilo.Amesema utaratibu wa kisheria utakapokamilika watu hao wanatarajiwa kupandishwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote