Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, February 19, 2010

China yalaani mkutano wa Obama na Dalai Lama

Wizara ya mambo ya nchi za nje ya China imelaani vikali mkutano uliofanyika kati ya Rais Barack Obama wa Marekani na kiongozi wa kidini wa jimbo la Tibet, Dalai Lama. Wizara hiyo imesema ilitarajia Marekani itachukua hatua za kuhakikisha inarejesha uhusiano wa nchi hizo mbili katika hali ya kawaida. Mazungumzo kati ya Rais Obama na Dalai Lama yalifanyika katika Ikulu ya Marekani-White House. China ilionya kuwa endapo mazungumzo hayo yatafanyika uhusiano kati ya nchi hizo mbili utaathirika zaidi. Hata hivyo vyombo vya habari havikuruhusiwa kuingia katika mkutano huo. Rais Obama alielezea nia yake ya kuiunga mkono Tibet katika kutetea na kulinda haki za kidini na kitamaduni za watu wa eneo hilo. Dalai Lama yuko katika ziara ya siku kumi nchini Marekani na anatarajiwa kutoa mihadhara itakayozungumzia kuhusu huruma na amani ya dunia huko California na Florida.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote