Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 18, 2010

Kuweni makini na Ombaomba

Pale salender Bridge ambapo anasimama trafiki akivuta magari, kuna mdada alikuwa ndani ya gari lake kwenye foleni akisubiri zamu yake ya kuruhusiwa na trafiki ifike apite. ndipo aliposogea kaka mmoja ombaomba, akasogea kwenye gari la yule dada na kuomba msaada. Dada huyo kwa kumhurumia akamsaidia. Alipompa pesa tu mkono wa yule dada ukaota manyoya ya paka, akachanganyikiwa alipokuwa anaendelea kushangaa trafiki akawa anaruhusu magari ya upande wake yule dada akawa hawezi kuendesha gari, ndipo trafiki akamsogelea na kuuliza kulikoni?! Yule dada akatoa mkono wake na kumuonyesha trafiki na kumsimulia kilichotokea na bahati nzuri yule kaka aliepewa pesa alikuwa mita chache pembeni anamuangalia yule dada. Ikabidi trafiki aende kumuuliza yule ombaomba kulikoni?Ndipo yule ombaomba akamwambia trafiki kuwa yule dada akimbusu tu atapona mkono utarudi kawaida. Basi ikabidi yule dada atelemke aende kumbusu yule kaka, alivyombusu wakapotea wote palepale, gari ya yule dada ikabaki barabarani ndipo trafiki alipoita watu wakaanza kuisukuma ile gari na kuiweka pembeni.Kuna dada mwingine alikuwepo leo kanisani baada ya ibada akawa anatusimulia, yeye alikuwa nyuma ya gari ya huyo dada alishuhudia hilo tukio anasema ni tukio la kweli kabisa ameshuhudia kwa macho yake.Hivyo jamani nawatahadharisha ndugu zangu mlio na moyo wa huruma msipende kutoa pesa zenu hovyo sababu umekutana na maskini.Biblia inasema maskini wapo na wataendelea kuwepo, mwombe Mungu kwanza kila unapotaka kutoa sadaka yako. Mwenye Masikio na Asikie

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote