Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, February 22, 2010

Happy Birthday Mugabe

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amesherehekea siku yake ya kuzaliwa na kufikisha umri wa miaka 86 na kuwa rais mzee kuliko wote duniani. Vyombo vya habari vya Zimbabwe jana jumapili vilimwagia pongezi na sifa kibao rais Robert Mugabe kwa kutimiza umri wa miaka 86.Mashirika yanayomilikiwa na serikali, makundi ya kanisa na baadhi ya mashirika binafsi yaliweka matangazo ya kurasa nzima kwenye magazeti kumpongeza Mugabe na kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.Mugabe ambaye amekuwa akiitawala Zimbabwe tangia mwaka 1980 alimiminiwa sifa kibao akitajwa kuwa yeye ndiye mtetezi wa kutokomeza fikra za kikoloni.Mugabe ambaye kwa sasa anapata upinzani mkubwa toka kwa kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai, aliitumia siku yake ya kuzaliwa kimya kimya akiwa na familia yake.Sherehe kubwa zitafanyika jumamosi ijayo mjini Bulawayo ambapo maelfu ya watu wataweza kujumuika na rais Mugabe kusherekea siku yake hiyo ya kuzaliwa.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote