Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, February 17, 2010

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Wanawake Chatangazwa

Adolf Rishard, Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya wanawake ya Twiga Stars itakayoshiriki katika michuano ya awali ya kufuzu kushiriki fainali za Afrika za wanawake nchini Afrika Kusini, ametangaza kikosi cha wachezaji 27 kitakachopambana na timu ya taifa Ethiopia.Mechi hiyo itachezwa Machi 6 mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.Adolf alitangaza majina hayo kwa niaba ya kocha mkuu Charles Boniface ambaye yupo nje ya jiji la Dar es Salaam.Wachezaji hao tayari wameingia kambini jana katika Hosteli ya Lamada iliyopo Ilala jiji Dar es Salaam.Adolf akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za Chama cha Mpira wa miguu nchini TFF alisema kuwa yeye kwa uhakika haifahamu timu ya Ethiopia lakini anacho jua ni timu nzuri na watahakikisha yeye na kocha wake mkuu wanafanya kila liwezekanalo katika kuwaandaa vijana wao Twiga stars wanaoendelea na mazoezi katika Uwanja wa Karume uliopo katika ofisi za TFF.Aliwataja wachezaji watakaoiwakilisha Tanzania kuwa ni Fatma Omari ,Pulkeria Chalaji, Sofia Mwasikila, Mary Masatu, Estar Chabuluma, Fatuma Mstafa, Zena Juma na Fatuma Bushiri.Wengine ni pamoja na Neema Kuga, Hindu Muharami, Aisha Rashidi, Fadhila Kilele, Mwanahamisi Omary, Fatuma Hatibu, Mwanaidi Temba, Zena Hamisi na Hellen Peter.Katika orodha hiyo pia wamo Pridian Daud Ettoo Mlezi, Fadhia Hamadi, Maimuna Said, Nasiria Ashri Abdallah, Mwajuma Abdalaah, Hakima Mwasilimu Hamis ,Warda Khalid Abdallah, Musimu Suluhu Hussan na Anita Elias.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote