Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 25, 2010

Ronaldo Kustaafu Mwakani?

Nyota wa Brazili, Ronaldo de Lima ametangaza mpango wake wa kustaafu kucheza soka mwakani. Ronaldo ambaye kwa sasa anaichezea timu ya Corinthians ya jijini Sao Paulo nchini Brazili, ametangaza kustaafu kucheza soka la kulipwa ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao. Ronaldo ambaye aliwahi kuchaguliwa mara tatu kuwa mchezaji bora wa dunia hivi sasa ana umri wa miaka 33. Ronaldo alisema kuwa atastaafu kucheza soka lakini ataendelea kuiwakilisha Corinthians baada ya kustaafu kama balozi wake. "Nimeongeza mkataba wangu kwa miaka miwili natarajia ndio miaka miwili ya mwisho katika soka", alisema Ronaldo. Ronaldo ambaye aliibeba Brazili kutwaa kombe la dunia mwaka 1994 na 2002 hakuweza kuyaficha matumaini yake ya kuitwa kwenye kikosi cha Brazili kitakachoshiriki kombe la dunia baadae mwaka huu nchini Afrika Kusini. "Tutaona itakavyokuwa, bado nina nafasi ya kuitwa timu ya taifa" alisema Ronaldo na kuongeza "Kwa kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazili itakuwa vigumu sana kwangu kushiriki kwani umri wangu utakuwa umesogea sana".

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote