Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 25, 2010

Lyon kuitibulia Simba rekodi?

AFRICAN Lyon imeungana na Kagera Sugar kutibua rekodi ya Simba ya ushindi wa mechi zote msimu huu baada ya kuibana na kutoka sare ya bao 1-1. Kwa matokeo hayo, Simba wamezidi kucheleweshewa hafla yao ya ubingwa ambayo ilihitaji ushindi wa mechi mbili pekee kabla ya mechi ya jana. Katika mchezo huo, Lyon, walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji Robert Ssentongo katika dakika ya 5 baada ya kupata krosi safi ya Hamis Shengo iliyomchanganya kipa Juma Kaseja wa Simba. wakati goli la Simba lilipatikana katika dakika ya 81, lilifungwa na Mgosi baada ya kupiga shuti kali lililompita kipa wa Lyon, Ivo Mapunda. Kwa matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 50 na kuiacha Yanga iliyo ya pili kwa pointi nane baada ya mwanzo wa wiki kuifumua Toto African kwa mabao 6-0.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote