Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, February 16, 2010

Hatimaye Wamarekani wamkamata Kamanda Mkuu wa Taliban

Kamanda mkuu wa kundi la Taliban,Mullah Abdul Ghani Baradar amekamatwa na maafisa wa ujasusi nchini Pakistan. Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la New York Times, maafisa wa Marekani wamethibitisha kwamba Mullah Abdul Ghani Baradar alikamatwa na maafisa wa ujasusi wa Marekani wakishirikiana na wenzao wa Pakistan. Mtu huyo anazuiliwa na maafisa wa Pakistan, Mullah Baradar ndiye anayeongoza harakati za kundi la Taliban nchini Afghanistan. Kamanda huyo ni mmoja wa viongozi katika baraza kuu la kundi hilo akishikilia wadhifa wa naibu kiongozi wa Taliban . Kiongozi mkuu wa Taliban Mullah Muhammad Omar ameendelea kuwa mafichoni.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote