Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, February 16, 2010

Hispania kuwachukua wafungwa kutoka jela ya Guantanamo?

Waziri wa mambo ya nje wa Uhispania Miguel Angel Moratinos amesema nchi yake iko tayari kuwapokea wafungwa watano kutoka jela ya Marekani ya Guantanamo Bay iliyoko katika kisiwa cha Cuba.Hata hivyo waziri huyo amekataa kusema wafungwa hao ni raia wa nchi gani . Kiasi cha nchi 10 wanachama wa Umoja wa Ulaya hadi sasa zimeridhia kuwapokea wafungwa kutoka jela hiyo.Mara ya kwanza Uhispania ilikubali kuwapokea wafungwa kutoka jela ya Guantanamo mwaka uliopita wakati uhusiano kati yake na Marekani ulipoanza kuimarika kufuatia ziara ya waziri mkuu Jose Luis Rodriguez Zapatero katika ikulu ya Marekani kwa mara ya kwanza tangu Uhispania ilipowaondoa wanajeshi wake nchini Iraq mwaka 2004. Uhusiano huo hata hivyo uliingia dosari mwezi huu baada ya rais Obama kusema hatohudhuria mkutano kati ya nchi yake na Umoja wa Ulaya unaotarajiwa kuandaliwa mjini Madrid mwezi Mei.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote