Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 25, 2010

Mkoa wa Morogoro kuwa na Majimbo mawili mapya?

BARAZA la madiwani wa Halmashauri ya Morogoro limepitisha mapendekezo ya kuligawa jimbo la Morogoro mjini ili liweze kuwa na majimbo mawili ya uchaguzi katika kurahisha huduma za maendeleo kwa wananchi. Akitangaza mapendekezo hayo katika kikao cha baraza la madiwani wa Manispaa ya Morogoro,meya wa Manispaa hiyo, Profesa Romanus Ishengoma alisema kutokana na mabadiliko hayo sasa kutakuwa na jimbo ya Bondwa na jimbo la Lupanga . Ishengoma alisema mabadiliko hayo yamelenga kuwarahisishia huduma za kijamii wananchi wa Manispaa ya Morogoro wanaokadiriwa kufikia 500,000. Alisema mbali na kupendekeza majimbo mawili pia baraza hilo la madiwani limependekeza kuongeza tarafa kutoka moja na kuwa mbili za Lupanga na Bondwa ikiwa ni pamoja na kuongeza kata za manispaa hiyo. Akisoma mapendekezo hayo katika kikao hicho,naibu meya wa manispaa hiyo, Amir Nondo alisema pia mapendekezo hayo yamelenga kuzigawa kata kutoka kata 19 hadi kufikia 26 kulingana na ukubwa wa baadhi ya kata. Nondo alizitaja kata zilizogawanywa kuwa ni pamoja na kata ya Mbuyuni ambayo itakuwa na kata mbili za Magadu na Mbuyuni,kata ya Mzinga itakayokuwa na kata ya Luhungo na Kauzeni na kata ya Mwembesongo itakayokuwa na kata ya Mafisa na Mwembesongo. Naibu meya huyo alizitaja kata zingine zilizopendekezwa kugawanywa kuwa ni kata ya Kihonda itakayokuwa na kata ya Kihonda na Mkundi,kata ya Kingulwira itakayokuwa na kata ya Tungi na Kingulwira na kata ya Mazimbu itakayokuwa na kata ya Mazimbu,Mindu na Magorofani.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote