Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 25, 2010

Mwanamke Aliyesingizia Kubakwa Atupwa Jela

Biurny Peguero mwenye umri wa miaka 27 mkazi wa jiji la New York nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela kati ya mwaka mmoja na miaka mitatu baada ya kukiri kumsingizia mwanaume asiye na hatia kuwa amembaka.Mwaka 2005, Biurny alimsingizia mwanaume huyo kuwa alimtishia na kisu kabla ya kumbaka. Mwanaume huyo alihukumiwa kwenda jela miaka minne.Mwaka jana Biurny alienda kutubu madhambi yake kanisani na kukiri mbele ya mchungaji kuwa alimsingizia mwanaume asiye na hatia kuwa amembaka.Hatua hiyo ilisababisha polisi wapewe taarifa ambapo mwanaume huyo aliachiliwa huru muda mfupi baadae.Akisomewa hukumu yake, Biurny alihukumiwa kwenda jela kutumikia kifungo cha kati ya mwaka mmoja na miaka mitatu.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote