Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, February 19, 2010

Manara akamatwa baada ya kutoroka

AMHAJJI MANARA, aliyekuwa Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, aliyekimbia baada ya kudhaminiwa katika Kituo cha Polisi Magomeni amekamatwa tena na anashikiliwa na Jeshi hilo kwa mahojiano . Awali, Manara alikamatwa Januari 28, mwaka huu baada ya kutuhumiwa kutapeli magari kwa kutumia jina la Chama Cha Mapinduzi.Baadaye alikimbia dhamana aliyowekewa na mama yake mzazi, hali iliyosababisha mama yake kukamatwa na kuswekwa rumande.Hivyo jeshi hilo lilifanya msako mkali na jana alikamatwa na kufikishwa tena katika kituo cha polisi cha Magomeni.Manara alidaiwa kukodisha magari zaidi ya 40 kutoka kampuni tofauti nchini za kukodisha magari kwa kutumia jina la CCM.Hata hivyo Jeshi hilo lilisema kutokana na kuwa Manara alishakiuka masharti ya dhamana na kuikimbia hawatamwachia tena hadi watakapompeleka mahakamani.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote