Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 25, 2010

Jaribio la ndege kulipuka lawashtua wengi Dar

Maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam, jana walipata mshtuko na kuanza kukimbia kwenda Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kungalia ndugu zao kama wapo hai baada ya kuwepo taarifa za kutokea ajali ya ndege katika uwanja huo na kuua abiria kadhaa.Mtafaruku huo uliotokea jana mchana na kusababisha vikosi vya ulinzi na usalama kutimua mbio huku vikiwa na ving'ora kuelekea uwanja huo kwa ajili kwenda kufanya kazi ya uokoaji.Hata hivyo, jambo la kushangaza baada ya vikosi hivyo kufika katika uwanja huo, viliambiwa kwamba hapakuwa na tukio lolote baya bali Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), iliamua kufanya maigizo yanayofanana na tukio la kweli la ajali.Akizungumza na vyombo vya habari, Kaimu Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Charles Kenyela, alisema hata yeye alipatwa na mshtuko mkubwa baada ya kupata taarifa hizo.Hata hivyo, alisema baada ya kufika eneo la tukio, alishangaa kuona halikuwa tukio la kweli bali yalikuwa maigizo kwa lengo la kupima utayari wa mamlaka husika endapo ajali ya ndege itatokea."Ni kweli na mimi nipo hapa lakini hakuna tukio baya na nimeambiwa haya ni maigizo ya kawaida ili kuviweka tayari vikosi vya ulinzi na uokoaji," alisema.Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Prosper Tesha, alisema zoezi hilo hufanyika mara moja kila baada ya miaka miwili.Alisema katika zoezi hilo wamegundua mapungufu makubwa katika upande wa usafiri kwa ajili ya kupitisha magari ya uokoaji kwenda Uwanja wa Ndege

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote