Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, February 16, 2010

Kifusi chaua watano - Dodoma

WATU watano wamefariki dunia papo hapo jana, baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakiwa wanachimba kokoto huko katika kijiji cha Ntyuka, mkoani Dodoma Waliofariki katika tukio hilo ni wanawake watatu na watoto wawili ambao walikuwa na mama zao eneo la tukio.Wanawake hao ni Monica Chizumi na mwanawe Porina Chizumi mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu, Mwajuma Mnubi na mtoto wake, Jonas Mnubi wa mwaka mmoja na miezi 8 na Mbeleje NdingomoMbali na waliokufa dunia watu wengine wawili ambao ni Beatrice Chizumi na Noel Lazaro alijeruhiwa na walikimbizwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya kunusurika katika tukio hilo.Tukio hilo la kusikitisha lililotokea jana majira ya saa 7 mchana kijijini humo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote