Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni! eti kuna tetesi kuwa hili neno la Wamachinga watu wanalielewa vibaya wabongo wengi wanafikiri kuwa wamachinga ni wale wafanyabiashara za mkononi hasahasa watu wanaotoka mikoa ya kusini, lakini ukweli ni kwamba biashara hizi hazifanywi na watu wanaotoka kusini tu ila watu wanaotoka mikoa mbalimbali katika nchi yetu
Wamachinga ni kabila mojawapo linalopatikana katika Mkoa wa lindi na jamii hii inapatikana katika maeneo ya Mchinga, mila na desturi za kabila hili hazina tofauti na watu wengine wanaotoka mikoa ya pwani.
Wabongo wengi wamelielewa Neno hili vibaya lakini kutokana na tembeatembea yangu mtaani inaonyesha walikuwa wanamaanisha (Maching - Guy) yaani wanafanyabiashara wanaofanya biashara za kutembea toka sehemu moja kwenda nyingine sasa wao baada ya kutamka Maching - Guy wanatamka Machinga ndio hapo watu wakaanza kusambaza uvumi huu na kusema wanaofanya biashar hizi ni watu kutoka kusini .
1 comment:
Hii nimeipenda, Sikuwahi kufikiria hili. Nilikuwa najua tu ya kariakoo
Post a Comment