Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, December 3, 2009

Rwanda Mwanachama mpya Jumuiya Madola

Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola wamepokea na kukubali ombi la Rwanda la kuwa mwanachama wa Jumuiya hiyo.Kutokana na uamuzi huo uliofikiwa jana kabla ya kufungwa kwa mkutano huo, Rwanda sasa inakuwa mwanachama wa 54 wa Jumuiya ya Madola. Rwanda ambayo haikutawaliwa na Uingereza inakuwa nchi ya pili baada ya Msumbiji kujiunga na Jumuiya ya madola ambayo inaundwa na nchi zilizokuwa makoloni ya Uingereza. Rwanda ilitawaliwa na Ubelgiji wakati Msumbiji ilikuwa koloni la Ureno. Tayari sekretarieti ya Jumuiya ya Madola imeshamuarifu Rais Paul Kagame wa Rwanda kuhusiana na nchi yake kukubaliwa kuwa mwanachama.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote